Kivu ya kaskazini : Liwali Costant Ndima Kogba atembelea askari jeshi na raia akiwapongeza kuhusu vita eneo hilo

Liwali Costant Ndima Kogba.

Liwali wa jimbo la Kivu ya kaskazini Costant Ndima Kogba ametembelea wilayani Rutshuru majuzi ili kuwapa moyo askari jeshi kwenyi vita, pamoja na hayo kupongeza wenyi majeraha ya vita, na raia kwa jumla wilayani humo.

Duru zaeleza kwamba liwali mwanajeshi alikutana pia na makamanda wa operesheni na baadae kwenda kutembelea wahanga wa majeraha za vita wenyi kuwa hospitalini.

Baada ya hapo liwali wa jimbo la Kivu ya kaskazini alijielekeza pa Rwanguba barabara inayopelekea pa Bunagana ambako alikutana askari jeshi wakiwa uwanjani. Hawa walihakikisha kupigania nchi, wakitowa maisha yao yote.

Jenerali Constant Ndima aliwashukuru kwa bidii, kutokana na hatua walioichukuwa ya kutumikia taifa nzima.

Chumba cha wandishi

Soyez le premier à commenter

Poster un Commentaire