« Tuna hamasisha raia kuhusu maendeleo ya kwetu Ijapo ukosefu wa vifaa . Tunafanya kila juma mosi kazi za salongo, tukifunguwa njia ndani ya eneo, Ijapo ukosefu wa vyombo vya Kazi. Kwa hiyo, tunaomba shirika zisizo za kiserkali pamoja na shirika la serkali husika na maendeleo Fonds social de la République, kutuunga mikono kwa vifaa il tufikie lengo , aeleza Kiongozi huyo.
Akizungumza n’a wandishi habari hii ijumaa tarehe 10 juni 2022, Riphin Kanuma Ndambi anena pia kwamba idadi ya wakàazi eneo Hilo yaomgezeka siku kwa siku. Wakàazi wahitaji nafasi ya soko il waepuke hatari wakichuuza kando ya barabara, Bila kusahau shamba la wafu, kwa kuwa Jambo hili lawakera kama viongozi wa mahali. Wakosa jibu kwa malalamiko ya raia mtu anapofariki ndani ya eneo.
Kuhusu maji safi, Kiongozi huyu aendelea kushukuru shirika Merci corps, ambalo lilisaidia raia kupata bomba kadhaa za maji ndani ya kijiji, hâta kama ombi ni kubwa. Ila upande wa moto wa umeme, shida ni kubwa mno. Wakàazi wapinga kuhudumiwa n’a shirika SOCODEE kuhusu beyi kali, wakihitaji kuhudumiwa na Virunga SARL kulingana na pato yao.
Juvénal Murhula.
.
Poster un Commentaire
Vous devez vous connecter pour publier un commentaire.