Ni mabwana Dédé Ndungi na Antoine Yoba, moja kwa moja Kiongozi nchini na Mratibu jimboni Kongo central kwenyi mpango husika na usafi mipakani nchini DRC, wahutumiwa.
Ni chumba husika na uchunguzi wa pesa, ndio kiliomba ndani ya barua kilichotuma kwa kiongozi mkuu husika na mambo ya wahami. Viongozi hawo husika wa mpango PNHF, wakatazwa kutoka nje ya nchi. Hiyo ni kulingana na kuzaniwa kupokonya mali ya uma.
Kutokana n’a barua hiyo iliyo chunguzwa na wapasha wa 7 sur 7. cd, uchunguzi uliofanyika kwenyi shirika husika na usafi mipakani pamoja na maoni kadhaa, yaonyesha kwamba kunazaniwa vitendo vya wizi ya mali ya uma.
Duru zaendelea kwamba barua kuhusu jambo hilo, itatumwa kwenyi vyombo vya sheria, ili kuanzisha mashtaka kwa wahutumiwa hawo wawili.
Tufahamishe kwamba shirika husika na usafi mipakani nchini PNHF ni shirika la serkali ya DRC, upande wa widhara ya afya. Tangu kuundwa kwake mwaka 2002, shirika hilo la husika na uchunguzi wa usafi mipakani nchini DRC. Likihusika pia na chanjo dhidi ya homa kali yaani fièvre typhoïde kwa kimombo, na kuorodhesha watu wa magonjwa kadhaa.
Juvénal Murhula.
Poster un Commentaire
Vous devez vous connecter pour publier un commentaire.