Goma: Patrick Mundeke alaumu vitendo vya kinyama humu jimboni ijapo kuweko walinzi wa usalama

Prezidenti wa vijana upande wake Moise Katumbi Patrick Mundeke.

Akitokea mjini Lubumbashi ambako alishiriki kwenyi uzinduzi wa ofisi ya chama Ensemble pour la République, Kiongozi wa vijana upande wake Moise Katumbi Patrick Mundeke aonyesha raia umuhimu wa kumcagua Moïse Katumbi. Akinena kuwa ataleta mapinduzi ndani ya siasa ya DRC, na ya uongozi wa nchi.

Patrick Mundeke alitaja mfano wa makao maalam ya chama Ensemble pour la République huko Lubumbashi, Kinshasa, Kisangani na hapa karibuni mjini Goma. Ijapo kuna vyamaa vilivyo tawala miaka thelasini na mbili, vingine miaka kumi na munane bila makao.

Kiongozi wa vijana wake Moïse Katumbi alilaumu pia vitendo vya kinyama wanavyo vitendea hata watoto wadogo. Akitowa mfano wa mtoto aliyetekwa nyara wakilazimisha jamaa dola elfu 2 za marekani, ambazo hazikupafikana.

Ndipo watenda maovu kumuuwa mtoto, akisema atajielekeza kwenyi kilio ili kupongeza jamaa la mtoto aliyeuliwa. Na kwamba mtu yeyote wa moyo mwema aweze kupongeza jamaa hilo mhang

Patrick Mundeke alaumu vitendo hivyo ijapo kuweko kwa askari jeshi na polisi mahali.

Juvénal Murhula

Soyez le premier à commenter

Poster un Commentaire